This Blog Publishes Records and Archives Management Mareials By, Hussein A.Rubaka Cantact him on +225717872020 or allyrubaka@gmail Or allyh41@yahoo.com, for assistance on this field. Also this Blog Publishes T.P.S.C News. @@ YOUR WELL COME @@
Saturday, March 21, 2015
YALIYO JILI KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI TANGA DHIDI YA YANGA & MGAMBO JKT.
Uwanja wa Mkwakwani Tanga leo palikuwa hapatoshi, Timu ya Yanga walikuwa wakipambana na Mgambo JKT ambao walikutana na timu ya Simba na kuwafunga 2-0, leo ilikuwa zamu ya Yanga na Mgambo.
Dakika 45 za kwanza ziliisha kwa 0-0 lakini waliporudi kumalizia 45 za kipindi cha pili hali ilikuwa tofauti, Yanga waliwazidi nguvu Mgambo na kumaliza dakika 90 za mchezo kwa goli 2-0 ambapo Yanga walitoka kifua mbele kuthibitisha kwamba bado wanahitaji kukaa kwenye kilele cha ligi Kuu Tanzania bara.
Niger yaomba msaada wa kuwahudumia wakimbizi
Viongozi wa Niger wametangaza kuwa, nchi hiyo
haina uwezo wa kuwahudumia wakimbizi wanaoingia nchini humo wakitokea katika
nchi jirani ya Nigeria. Maafisa wa serikali ya Niger wanasema, wimbi la
wakimbizi wanaoingia nchini humo limekuwa kubwa mno kiasi cha kushindwa nchi
hiyo kukabiliana nalo. Taarifa zaidi zinasema kuwa, Niger imeiomba jamii ya
kimataifa iisaidie ili iweze kuwahudumia wakimbizi hao. Taarifa ya serikali ya
Niger imebainisha kwamba, inaitaka jamii ya kimataifa iisaidie chakula, ujenzi
wa makazi ya muda na huduma za kitiba na kiafya. Wimbi la wakimbizi wanaoingia
nchini Niger limeifanya nchi hiyo ikabiliwe na hali mbaya zaidi hasa kwa
kuzingatia kwamba, nchi hiyo yenyewe ni miongoni mwa nchi masikini zaidi
duniani na imekuwa ikitaabika kwa ukame na majanga mbalimbali ya kimaumbile.
Wakimbizi hao wamekuwa wakiingia Niger kutokea Nigeria wanakokimbia mashambulio
ya kundi la kigaidi la Boko Haram. Mashambulio ya kundi la Boko Haram la
Nigeria yamepanuka zaidi na kutishia usalama wa raia katika nchi jirani na nchi
hiyo ikiwemo Niger, Cameroon na hata Chad. Nchi jirani na Nigeria tayari
zimeunda kikosi cha pamoja cha kukabiliana na wanamgambo wa Boko Haram.
Subscribe to:
Posts (Atom)